$type=slider$snippet=hide$cate=0

Utoro, vilaza ni matokeo ya utitiri darasani

Na Komba Kakoa IMEELEZWA kuwa utitiri wa wanafunzi katika madarasa umekuwa ukichangia  kushusha kiwango cha ubora wa elimu inay...



Na Komba Kakoa



IMEELEZWA kuwa utitiri wa wanafunzi katika madarasa umekuwa ukichangia  kushusha kiwango cha ubora wa elimu inayotolewa kwa wanafunzi wa msingi na sekondari hapa nchini.
Hili linatokana na ukweli kwamba madarasa yenye msongamano wa wanafunzi yamekuwa mzigo mkubwa kwa walimu wanapofundisha  hali inayowafanya kushindwa kueleweka kwa wanafunzi wote kwa wakati mmoja.
Mbali na hiyo, mwalimu anayefundisha katika madarasa yenye wanafunzi wengi imampa wakati mgumu kuweza kujua tabia za kila mwanafunzi na hasa pale anapotaka kupima maendeleo ya mwanafunzi mmojammoja.

Kutokana na hali hiyo wadau wa maswala ya elimu wanasema kwamba madarasa yenye msongamano wa wanafunzi yanachangia walimu kushindwa kutekeleza vizuri malengo yao ya kutoa elimu kwa vitendo.
Wanafunzi wakiwa wamejazana darasani huku wengine wakikaa chini kutokana na ukosefu wa madawati hali ambayo inaathiri uelewa wa mwanafunzi pamoja na ufundishaji wa mwalimu.

Kadhalika wadau hao wanasema kuwa mwalimu anayefundisha katika madarasa  ya aina hiyo anatumia muda mwingi katika kufundisha somo lake na kuhakikisha kila mwanafunzi anayehudhuria kipindi chake ameelewa.
Stephen Kika, ni mwalimu wa shule ya Msingi Mgambo, iliyo katika wilaya ya  Kilindi Mkoani Tanga anasema hali hii husababisha mwalimu kushindwa kudhibiti wanafunzi wake.
Kika ambaye pia ni mwalimu wa Taaluma katika shule hiyo anasema kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya wanafunzi katika chumba cha darasa humwia ngumu mwalimu kubaini tabia za wanafunzi wote hasa walioketi viti vya nyuma au walio kosa kabisa,”nasema Mwl. Kika.
“Madarasa ya aina hii yanahitaji jitihada kubwa ya mwalimu katika kudhibiti muda wa ufundishaji, kwasababu humlazimu mwalimu kutumia muda mwingi  katika kufundisha mada moja,”Anasema Mwl. Kika.
Kwa upande wake Mwalimu Aisha Hemed, ambaye pia ni mwalimu anasema idadi kubwa ya wanafunzi na ukubwa wa madarasa, huwakosesha walimu wasiweze kuwa  na ari pamoja na nguvu ya kufundisha.
Mwl. Aisha ambaye pia ni Mkurugenzi wa shirika lisilo la Kiserikali la Youth for Development (Y4D) anasema kuwa hali hiyo haimuathiri mwalimu pekee bali huathiri tabia na usomaji wa mwanafunzi pia kwa kumfanya asijishughulishe zaidi katika masomo na shughuli za kijamii kwa ujumla.
Mwl. Aisha anasema kuwa katika ufundishaji, usikivu wa wanafunzi darasani ni jambo la muhimu linalopaswa kupewa kipaumbele kutokana na ukweli usiopingika kwamba unaathiri ushiriki wake katika masomo.
“Utafiti unaonyesha kuwa madarasa yenye watu wachache wanafunzi wanatumia muda mchache kufanya mazoezi yao na yanatoa nafasi kufanya mazoezi mengi zaidi pia wana uwezo wa walimu hupata fursa ya kuwa karibu na watoto wote na kuwafanya wawajibike kuliko  kuwadharau wanafunzi wenye uwezo mdogo kiakili darasani.
Hata hivyo Mwl. Aisha anaukosoa mfumo uliopo kwamba kumekuwa na tabia ya ujengaji wa madarasa makubwa yenye wanafunzi wengi huku wakitegemea kupata ufundishaji unaokidhi viwango katika hali ya juu na dira ikiwa ni elimu kwa vitendo zaidi.
Yosepha Hokororo, mwalimu mstaafu wa shule ya msingi Mkoani Lindi anasema kuwa madarasa yenye wanafunzi wengi yanamnyima fursa mwalimu ya kujua tabia ya mwanafunzi binafsi kutokana na ufinyu wa muda ukilinganisha na idadi yao.
“Wanafunzi wakiwa wengi kupita kiasi katika darasa moja, wanafunzi wanashindwa kumsikiliza mwalimu aliye mbele kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo usikivu mdogo hasa kwa waliokaa viti vya nyuma ama waliokosa viti kabisa,” Mwl. Hokororo.
Akitolea mfano katika shule mbalimbali za vijijini, Mwl. Hokororo anasema kuwa kuna shule nyingi ambazo hazina walimu wakutosha hali ambayo huwafanya walimu kutumia mbinu zisizo rasmi katika ufundishaji kwa wanafunzi wao.
“Uwiano uliopo ni mwalimu mmoja kwa wanafunzi 125 kwa wakati mmoja ukiacha mikondo mingine, inamuwia vigumu kusimamia utaratibu na  wakati mwingine zoezi la kuweka kumbukumbu za wanafunzi linashindikana,”Anasema.
Akizungumzia utendaji wa mwanafunzi mmojammoja, Mwl. Hokororo anabainisha wazi kuwa katika darasa lenye  idadi kubwa ya wanafunzi  hakuna  upimaji mzuri wa maendeleo ya wanafunzi  kutokana na ukweli kuwa mwalimu anaelemewa na  kazi nyingi  za kufanya ikiwemo kuhifadhi kumbukumbu ya kila mmoja.

ATHARI  KISAIKOLOJIA
Kwa mujibu wa Mwl. Hokororo, asilimia 20 ya wanafunzi walioko darasani ndio wenye uwezo wa kuuliza maswali jambo linalosababishwa na ukosefu wa mwingiliano kati ya walimu na wanafunzi kutokana na majukumu mengi.
 “Hali hiyo inachangia kushusha ujuzi wa mwalimu kwakuwa anakosa muda wa kutosha kusoma, kusikiliza, kubadilishana mawazo pamoja na kufuatilia wanafunzi jambo ambalo humfanya mwalimu ashindwe kufahamu upekee wa mwanafunzi wake,”Anasema.
Anaongeza kuwa katika hali ya kawaida  madarasa kama haya huwa na mwingiliano mkubwa baina ya walimu na wanafunzi, hivyo ni wanafunzi  wachache tu ndio wanaopata nafasi ya kuuliza ama kujibu maswali.
Aidha, mstaafu huyo, anasema kuwa kutokana na hali halisi mwalimu anakosa nafasi ya kukagua maendeleo ya mwanafunzi mmojammoja na kugundua yupi anahitaji msaada wake wa karibu zaidi.
“Unakuta tangu umeingia darasani na kufundisha hadi unatoka kati ya wanafunzi 78, walioko darasani 20, tu wameuliza maswali na kujibu hali hiyo huchangia wanafunzi wenye uwezo mdogo wa kuelewa kudharaulika kutokana na walimu wao kuwa na shughuli nyingi katika kufundisha jambo ambalo huwafanya wazidi kuwa dhaifu zaidi,”Anabainisha.
“Madarasa yenye msongamano yana madhara makubwa kwa wanafunzi kutokana na ukweli kuwa unapunguza nafasi kwa shule kutoa elimu bora nchini,”.
Naye Sebastian Namihambi, ambaye pia ni mwalimu mstaafu anasema ni vigumu kwa mwalimu kufanya uchambuzi wa wanafunzi binafsi kwasababu jambo hilo linahitaji muda zaidi.
Namihambi anasema kuwa kutokana na wingi wa wanafunzi darasani, wachache kati yao ndio hupata msaada wa mwalimu pindi wanapouhitaji lakini kadri wanavyoendelea kushindwa hujijengea tabia ya kuchukia shule na kuamua kutoroka ama kukaa nje ya madarasa.
“Kweli walimu wanapata wakati mgumu sana hasa wanapotaka kusimamia na kufundisha madarasa yenye wanafunzi wengi kwasababu kuwa wakati mwingine wanashindwa kutumia  mbinu mbalimbali za kufundisha,” anasema Sebastian.
Sebastian anafafanua zaidi kwamba hata pindi mwalimu anapoamua kutumia mbinu mbalimbali za kufundisha inakuwa ngumu   kwenye madarasa yenye msongamano jambo ambalo hukwamisha elimu hiyo kuwafikia wanafunzi wote kwa kiwango sawa.
Anasema kuwa kutokana wingi katika madarasa walimu wanashindwa kutumia mbinu za ziada kuleta ufanisi ikiwemo wanafunzi kupata nafasi ya kuuliza ama kujibu maswali wakati wa kipindi.
“Licha ya kusindwa kuelewa lakini pia ni hatari kwa afya kwasababu ufundishaji katika madarasa yaliyofurika  unaweza kusababisha mzunguko wa hali hewa kutokuwa mzuri hivyo kuchangia magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya hewa,” anasema Sebastian.
Anaongeza kuwa idadi kubwa ya wanafunzi isiyo na uwiano na uwezo wa darasa inaathiri uwezo wa wanafunzi kufuatilia kwa umakini ikiwemo kusikia na kusoma na kusababisha matokeo duni.
“Ni vigumu kwa mwanafunzi kutumia vifaa kwa vitendo kwa sababu hakuna uwiano uliopo baina ya wanafunzi waliopo darasani na vifaa vya kufundishia vinayotumiwa na mwalimu” Anafafanua.
“Uwiano wa idadi ya wanafunzi ambao uliwekwa kipindi cha nyuma na iliyokuwa Wizara ya Elimu na Utamaduni wa 1:40 ulidharauliwa, hivyo ni dhahiri kwamba hakutakuwa na mafanikio mazuri wala usimamiaji mzuri wa nidhamu.
Kutokana na hali hiyo Zainab Rashid, ambaye ni Mhadhiri msaidizi wa chuo cha Ustawi wa Jamii anasema ipo haja kwa serikali kuweka vipaumbele katika ujenzi wa miundombinu ya elimu pamoja na vitendea kazi.
Anasema ili mtoto aweze kujifunza vizuri ni lazima kuwe na mahusiano mazuri katika jamii jambo ambalo litaweza kumsaidia kwa kisai kikubwa.
Mwanasaikolojia huyo anasema kisaikolojia mwanafunzi hujifunza vizuri kwa kushirikiana na wenzake darasani wakiwa wachache jambo ambalo humpa fursa mwalimu kufuatilia maendeleo yao.
“Ukifundisha wanafunzi wachache huku ukiwagawa katika makundi wakashiriki vizuri inasaidia kuwajengea uwezo wa kufanya vizuri kwani mwanafunzi asiposhirikishwa huathirika kisaikolojia na kushindwa kuelewa anachofundishwa jambo ambalo humfanya akate tamaa,” anasema.
Anasema hali ya wanafunzi kushindwa kuelewa wanachojifunza kutokana na idadi kubwa darasani humuatthiri walimu anayewafundisha.
“Wanafunzi wasipoelewa mwalimu hukata tamaa ambapo wengine huacha kazi na kuamua kufanya mambo mengine lakini wanafunzi wakiwa wachache humfanya anayewandisha kuhamasika zaidi,”
Kutokana na hali hiyo anasema serikali inapaswa kuandaa mazingira mazuri ya kusomeshea wanafunzi ili waweze kujifunza na kuelewa vizuri.

NINI KIFANYIKE
Ili kuboresha elimu kuelekea Tanzania tunayoitaka ipo haja kwa serikali kuongeza nguvu katika kuwekeza kwenye seta ya elimu hususan kuboresha miundombinu na mazingira rafiki kwa watoto ili kuwawezesha kujifunza kwa nadharia na kwa vitendo.
Hii ina ukweli kwamba mazingira, miundombinu na idadi ndogo ya wanafunzi darasani humfanya mwanafunzi ajifunze na kuelewa vizuri na kumfanya mwalimu ahamasike na kuifurahia kazi yake,”
Mwanasaikolojia huyo anasema wazazi hupeleka watoto wao kwenye shule za watu binafsi kutokana na miundombinu rafiki iliyopo ambayo huwapa watoto fursa kujifunza kwa nadharia na vitendo zaidi juambo ambalo huongeza kiwango cha ufaulu.
Pia anasema serikali inalo jukumu la kuongeza walimu wa kutosha katika shule zake kwani inaelezwa kuwa jumla ya walimu waliopo ni 88,999 ambapo kati yao 18,545 hufundisha masomo ya sayansi huku 70,454 wakifundisha masomo ya sanaa na biashara.
Kuongeza idadi ya walimu kutapunguza mzigo wa kufundisha masomo mengi hivyo watakuwa na muda wa kutosha kufuatilia maendeleo na kufanya tathmini kwa wanafunzi wao.
Kadhalika wazazi nao hawapaswi kukwepa jukumu la kujenga ushirikiano wa karibu na walimu kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya watoto wao katika kujifunza kwao.
====================== 


COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Utoro, vilaza ni matokeo ya utitiri darasani
Utoro, vilaza ni matokeo ya utitiri darasani
https://3.bp.blogspot.com/-J8fl7nIqvGQ/V77QRNdTc0I/AAAAAAAAALg/_Nk-VaiJBZMaetHePzRdgGjePxmznAx0gCLcB/s400/Wanafunzi.JPG
https://3.bp.blogspot.com/-J8fl7nIqvGQ/V77QRNdTc0I/AAAAAAAAALg/_Nk-VaiJBZMaetHePzRdgGjePxmznAx0gCLcB/s72-c/Wanafunzi.JPG
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2016/08/utoro-vilaza-ni-matokeo-ya-utitiri.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2016/08/utoro-vilaza-ni-matokeo-ya-utitiri.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy