$type=slider$snippet=hide$cate=0

Wafanyabiashara Moro kuinyima kura CCM baada ya kupokonywa vibanda

 MKOA wa Morogoro ni mojawapo ya maeneo hapa nchini yanayokua kwa kasi kiuchumi kupitia shughuli za uzalishaji mali, kilimo na biashara...

 MKOA wa Morogoro ni mojawapo ya maeneo hapa nchini yanayokua kwa kasi kiuchumi kupitia shughuli za uzalishaji mali, kilimo na biashara na hivyo kuwa miongoni mwa maeneo hapa nchini yanayochangia uchumi wake katika pato la Taifa.
Tathmini inaonyesha kuwa ukuaji wa uchumi mkoani humo unakwenda sambamba na ongezeko la watu na hivyo kuwapo kwa hitaji kubwa la mazingira yanayorahisisha utekelezaji wa shughuli za uzalishaji na uendeshaji wa biashara hasa kundi kubwa la wafanyabiashara ndogondogo, maarufu kama wamachinga.
Pamoja na mchango mkubwa wa biashara ndogo ndogo kufikia wastani wa zaidi ya ajira milioni 5 hapa nchini, wafanyabiashara mkoani Morogoro na maeneo mengine nchini wanakabiliwa na tatizo la maeneo ya kuendesha biashara zao.
Pamoja na changamoto hiyo, migogoro kati ya wafanyabiashara ndogondogo na mamlaka imetajwa kuwa kikwazo cha maendeleo ya biashara ndogondogo mkoani humo.
Chanzo cha mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka miwili sasa kimetajwa kuwa ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Morogoro kuwataka wafanyabiashara wanaoendesha shughuli zao kwenye  eneo la Sabasaba, Halmshauri ya Manispaa ya Morogoro kukilipa chama hicho kodi ya pango huku wafanyabiashara hao wakigoma kwa maelezo kuwa eneo hilo sio mali ya CCM.
Wafanyabiashara hao zaidi ya 50 wanakilaumu CCM wilayani humo kuwa chanzo cha umasikini kwa kuzusha migogoro ambayo imesababisha wafanyabiashara wengi kukosa haki ya kufanya shughuli zao kwa uhuru, huku wakimtupia lawama Katibu wa CCM wilayani humo Ally Issa.
Wanamlalamika kutumia cheo chake kuwanyang’anya mabanda yao  ya biashara jambo ambalo limewaathiri kwa kiasi kikubwa katika shughuli zao.
Wanadai kuwa walipatiwa eneo hilo na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutokana na maeneo hayo kuwa wazi ambapo kwa makubaliano maalumu waliridhiana na uongozi wa Manispaa ya hiyo kujenga mabanda na kuendesha biashara zao kwenye maeneo rasmi baada ya wafanyabiashara wengi kulazimika kuendesha biashara zao kwenye maeneo yasiyoruhusiwa kwa kukosa maeneo ya kufanya biashara zao.
Wanasema katika hali ya kushangaza uongozi wa CCM wilaya ya Morogoro mjini walifika kwenye eneo hilo na kuanza kuwatoza kodi  huku wakitishia kuwafukuza wafanyabiashara watakaokaidi ikiwa ni pamoja na kunyang’anywa mabanda wanayoyatumia kuendesha biashara zao.
Akizungumzia kadhia hiyo kiongozi wa wafanyabiashara hao Robert Mluge anasema waliazimia wote kugoma kutozwa kodi kwa maelezo kuwa maeneo hayo ya wazi ni mali ya serikali na yanasimamiwa na Manispaa ya Morogoro na siyo mali ya CCM kama uongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya unavyodai.
“Katibu wa wilaya wa CCM alivyoona tumegoma kulipa kodi, walikuja na kuamuru kufunga mabanda yote, baada ya siku chache Katibu Ally alitoa amri yavunjwe ili CCM itafute watu wengine na kuwapa maeneo hayo… kwa kweli tuliumia sana,” anasema Mluge.
Anasema kuwa watekelezaji wa agizo hilo waliuza mali za wafanyabiashara zilizokuwamo ndani ya mabanda huku CCM ikiyakodisha kwa wafanyabiashara wengine kwa nguvu.
 “Sisi tuliingia makubaliano na Halmashauri ya Manispaa tukapewa maeneo tujenge mabanda yetu lakini tulitakiwa tutumie gharama zetu kwanza kujenga uzio kabla kufanya jambo lolote ili kuimarisha usalama wa eneo hilo lakini cha kushangaza CCM waliingilia jambo hili pasipo sababu za msingi,” alisema Mluge.
Mluge anasema katika kutafuta haki walifungua kesi katika mahakama ya ardhi dhidi ya CCM wilayani hapo ambapo wafanyabiashara walishinda kesi hiyo. Hata hivyo pamoja na ushindi huo CCM walipuuza hukumu ya mahakama ya kuwataka kurudisha vibanda hivyo kwa wafanyabiashara wenye haki. Hadi sasa mabanda hayo yanaendelea kushikiliwa na wafanyabiashara waliowekwa na CCM.
 Anasema baada ya kuona kila njia wanayotumia kutatua tatizo hilo inakwama, waliamua kumtumia barua Katibu Mkuu wa CCM taifa, Abdulrahman Kinana ili aimuru CCM wilayani humo kuheshimu sheria na mahakama lakini hadi sasa hakuna ufumbuzi wowote.
“Maisha yetu na familia yanalikuwa yakitegemea vibanda tulivyonyang’anywa, hivi sasa tunakosa ada ya shule kwa watoto wetu, mahitaji ya msingi nyumbani na mengine ya kijamii,” analalama Mluge. 
Mfanyabiashara mwingine, Lazarus Mizambwa anasema imekuwa ni jambo la kushangaza kwa chama ambacho kinasema sera zake ni za kuondoa umasikini kikiwa mstari wa mbele kuwakandamiza wafanyabiashara wadogo ambao wamekuwa muhimu kwenye maendeleo ya jamii na pato la taifa kwa ujumla.
 “Inashangaza sana, hiki ndicho chama ambacho kinaiaminisha jamii kwamba kina sera nzuri za kupunguza au kuondoa umasikini kwa kuandaa mkakati wa kukuza uchumi na kuondoa umasikini (Mkukuta), lakini kinaibadili mikakati hiyo ya kuongeza umasikini kwa wananchi kama hivi,” anasema Mizambwa.
Naye Flexon Lauo anasema kitendo hicho cha kibabe cha kunyang’anywa maeneo yao ya biashara kinawafanya wana jamii kupoteza imani na chama hicho kikongwe  hapa nchini.
 “Kama Manispaa ya Morogoro ambayo ndio imetupa maeneo haya ili kujikwamua kiuchumi, inakuwaje chama ambacho manispaa hii ni sehemu ya idara zake kinaipuuza manispaa na kutumia ubabe? Alihoji Lauo na kuendelea: Sisi tuliingia makubaliano na manispaa kwa nini wao waje baadaye na kuanza kutusumbua mbona hawakuja wakati tumeanza ujenzi? Huu ni uonevu maana wanatumia nguvu ya chama chao kunyanyasa wananchi, hatukubali na lazima kieleweke.
Anasema wafanyabiashara walitumia gharama nyingi kujenga mabanda hayo, hivyo kitendo cha kunyang’anywa na kuachwa bila shughuli ya kufanya  haiwafanyi kuendelea kukiamini CCM,  na kusema kwa umoja wao na watu wengine watakaowashawishi watavipigia kura vyama vya upinzani.
“Hatuwezi kukichagua chama ambacho kinaleta mateso kwa wananchi wake…kura zetu hawataziona na msimamo wetu uko pale pale kwamba lazima warudishe mabanda yetu na gharama tulizotumia kwenye ujenzi.”
 Anasema baada ya banda lake kubomolewa alipoteza mashine za kukoboa mahindi, mpunga na gunia 100 za mahindi na mali nyingine zilizokuwapo ndani ambazo mpaka sasa hazijapatikana na kudai kwamba CCM waliziuza.

NINI KILIO CHAO KWA SERIKALI?

Kilio chao ni kuona Serikali ikiingilia mgogoro huo kwani wafanyabiashara hao ni walipakodi wazuri ingawa serikali inatambua changamoto hiyo bila kuchukua hatua. 
Mluge anasema wana mpango wa kuwasiliana na wanasheria ili kuona haki ya wafanyabiashara wote inatimizwa.

MKURUGENZI WA MANISPAA:

Manispaa ya Morogoro ambayo wafanyabiashara hao wanadai maeneo waliyopokonywa waliyapata kutoka uongozi wake, Mkurugenzi wa Manispaa  hiyo, Theresia Mahongo anasema hana muda mrefu tangu ahamishiwe kituo hicho kipya cha kazi lakini atafuatilia na kutoa majibu.
“Ni kweli sisi ndiyo wenye mamlaka kwenye manispaa hii lakini mimi sina muda mrefu tangu nihamishiwe hapa, hivyo sina taarifa kuhusu jambo hili, ninachofahamu ni kwamba sabasaba ni eneo lililotengwa kwa ajili ya wafanyabiashara lakini huo mgogoro siufahamu…labda nitafuatilia alafu nitakupa majibu,” anasema Mahongo.
Hata hivyo amewataka wafanyabiashara hao kufika ofisini kwake kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao na kuahidi kuchukua hatua haraka kwani ni jukumu la manispaa husika.

MAJIBU YA CCM:

Mwandishi alimtafuta Katibu wa CCM wilaya ya Morogoro mjini, Ally Issa Ally ambaye malalamiko mengi yameelekezwa kwake, ambapo akizungumza kwa njia ya simu alipoulizwa kuhusu suala hilo alijibu kwa mkato kuwa hafahamu kuwa CCM ina mgogoro na wafanyabiashara.
Majibu yake ya mkato alipoulizwa na mwandishi yalikuwa hivi:
Mwandishi: Bila shaka wewe ni ndugu, Ally Issa Ally
Katibu: Ndiye mimi unasemaje?
Mwandishi: Unatambua mgogoro baina yenu CCM na wafanyabiashara wadogowadogo pale eneo la Sabasaba?
Katibu: Sifahamu lolote, kama unahitaji maelezo zaidi njoo ofisini
Mwandishi: Umesema hufahamu lolote, huko ofisini kuna maelezo gani zaidi?
Katibu: Kisha akakata simu.
Katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana hakupatikana kuzungumzia kadhia hiyo baada ya simu yake ya mkononi kutafutwa mara kwa mara bila kupokelewa au hapatikani wakati mwingine.
Wakati wafanyabiashara hao na wengine nchini wakiwa kwenye mazingira magumu kama hayo, serikali inakiri kuwa sekta ya viwanda vidogo na biashara ndogondogo zina mchango mkubwa katika ajira kwa takriban ajira 5,000,000 sawa na asilimia 23.4.
Kwa sasa sekta hiyo imechangia asilimia 27.9 katika pato la taifa ukilinganisha na mwaka 2012/13 ambapo sekta ya biashara ndondogo na viwanda vidogo imechangia asilimia 12.3.
Serikali kupitia wizara ya viwanda, biashara na masoko inasema ongezeko la ukuaji na uchangiaji huo umetokana na kuongezeka kwa fursa mbalimbali za masoko kwa bidhaa na uboreshaji wa mazingira ya kibiashara katika masoko ya ndani na nje ya nchi hasa kwenye nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC,  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC,  Jumuiya ya Ulaya, EU, Asia, Marekani na mashariki ya mbali. 

CHANZO: TAIFA LETU

COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Wafanyabiashara Moro kuinyima kura CCM baada ya kupokonywa vibanda
Wafanyabiashara Moro kuinyima kura CCM baada ya kupokonywa vibanda
http://2.bp.blogspot.com/-_ux-golSRKU/VdNUvgb5ILI/AAAAAAAAACI/-ZdKZJKS1_A/s320/Kinana.jpg
http://2.bp.blogspot.com/-_ux-golSRKU/VdNUvgb5ILI/AAAAAAAAACI/-ZdKZJKS1_A/s72-c/Kinana.jpg
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/08/wafanyabiashara-moro-kuinyima-kura-ccm_18.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/08/wafanyabiashara-moro-kuinyima-kura-ccm_18.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy