$type=slider$snippet=hide$cate=0

Njovu: Mwalimu msataafu anayeishi kwa kuchonga mihuri

           NA DODI SIFI ULE msemo usemao ‘Kupiga ndege wawili kwa jiwe moja’ unaendelea kuishi katika jamii zetu ambapo ni dhahiri ...

           NA DODI SIFI



ULE msemo usemao ‘Kupiga ndege wawili kwa jiwe moja’ unaendelea kuishi katika jamii zetu ambapo ni dhahiri unasadifu maisha ya Peter Njovu mwenye miaka 86 kutokana na jinsi anavyoendesha maisha yake.
Njovu ambaye alizaliwa mwaka 1930 kila siku asubuhi hukaa kibarazani kwake kuota jua kwa ajili ya kupata Vitamini D huku akichonga mihuri kazi anayoifanya kwa ustadi mkubwa ukilinganisha na umri wake na kujipatia fedha za kuendesha maisha yake.

Peter Njovu linaweza likawa si jina geni kwa walimu na watumishi wa serikali wa miaka ya 1970 na 1980. Alikuwa mtumishi wa serikali katika sekta ya elimu (mwalimu) tangu mwaka 1954 kabla ya kupanda ngazi na kuwa mratibu wa vyuo vya ufundi Tanzania katika kipindi cha miaka mitatu kutoka 1973 hadi 1976.
Mzee Njovu akiendelea na kazi ya kuchonga mihuri huko Kibamba jijini Dar es Salaam

Njovu pia ni msanii wa uchoraji na aliwahi kuchora picha maarufu ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambayo huonekana katika ofisi za Umma na hoteli mbalimbali. Tunaweza kusema mzee huyu amaeacha alama nzuri katika Taifa la Tanzania.
 “Kazi hii ya uchongaji na uchoraji nilianza nikiwa mdogo kabla sijaenda shule. Baada ya kustaafu kazi ya ualimu, nilianza tena uchongaji wa mihuri kutokana na ukiwa nilionao, mke wangu ameshafariki, watoto wangu wote wana miji yao, naishi peke yangu.
Kazi hii naichukulia kama sehemu ya kuondoa ukiwa lakini pia inanipatia pesa nzuri tu. anasema kwa masikitiko.
Siwezi kukaa bila kufanya kazi, kazi zote ndani ya nyumba yangu nazifanya mimi, usafi, kupika, hata kulima. Nikiwa na muda wa mapumziko nachukua kitabu au gazeti nasoma, hii ni kutokana na tabia niliyojijengea awali nikiwa mwanafunzi hata nilipokuwa mwalimu”.
 “Mimi nilichelewa sana kuanza shule kutokana na uchache wa shule pamoja na wazazi wetu kutokuwa na hamasa ya kupenda kuwapeleka watoto shule. Walipenda watoto wafanye kazi za mashambani na kutunza mifugo.
Anasema kilichomfanya aandikishwe shuleni ni kutokana na kipaji alichonacho hususan katika sanaa ya uchongaji na uchoraji. “Nikiwa kijana wa miaka 10 nilianza kuchonga vinyago na kuchora fani ambayo nimezaliwa nayo,Kutokana na umahiri wangu katika sanaa ya uchongaji na uchoraji , bidhaa zangu zilipendwa sana na Wazungu waliokuwa wafanya kazi katika misheni ya Peramiho ambao ndio walikuwa wateja wetu,”.
Kwa mujibu wa mzee Njovu wazungu hao walivutiwa na sanaa yake na kuamua kufika nyumbani kwao kwa lengo la kuwashawishi wazazi wampeleke shule kuendeleza kipaji chake ambapo walikubali”. Anasema.
Anasema baada ya wazazi wake kuridhia ombi la wazungu mwaka 1945 alianza darasa la kwanza katika shule ya msingi Peramiho akiwa na miaka 15.
“Kutokana na umri mkubwa ilibidi nirushwe darasa la kwanza na la pili ambayo alisoma kwa mwaka mmoja, pia sikuweza kusoma na kuandika vizuri,lakini nilikuwa nafanya mitihani na kufaulu vizuri darasani kwasababu nilikuwa na changamoto kubwa ya kushindwa kujieleza kwa kujibu maswali badala yake nilitumia sanaa yangu ya uchoraji kujibu maswali, na nilikuwa nikijibu kila mtihani kwa kutumia picha,”.
Anasma mwaka 1948 kati ya wanafunzi 32 walifanya mtihani wa darasa ya nne waliofaulu walikuwa wanne tu Njovu akiwa mmojawapo na kumfanya kuchaguliwa kujiunga na chuo cha ufundi hapo hapo Peramiho mwaka 1951 ambapo alisomea masomo ya uchongaji, uchoraji, useremala, na ufinyanzi.
1951-1953 alijiunga na chuo cha ualimu Peramiho ngazi ya diploma  na alipomaliza tu akaanza kufundisha chuoni hapo (1954).
“ Mimi nilikuwa mwalimu tofauti sana nilikuwa napenda kubadilisha mazingira ya kutoa elimu yangu, nilikuwa naomba serikali inihamishie katika shule za awali, msingi na vyuo vya ufundi, hii ni kutokana na mapungufu yaliyokuwa yanajitokeza katika sehemu nyingi na kuhitaji kupatiwa ufumbuzi wa haraka. Nilikuwa nazunguka mikoa ambayo ilikuwa nyuma kielimu, ili kubadilisha hali hiyo”
Baadhi ya vyuo alivyowahi kufundisha ni Chuo cha Ualimu Katoke, Kasulu, Mpwapwa, Tabora, Mara na Tanga.
Anasema mmoja wapo kati ya wanafunzi aliowafundisha ni jaji mkuu mstaafu wa Tanzania Barnas Samatta.
Pia Njovu anasema mwaka 1970 alipata ufadhili wa kwenda kusoma Korea Kaskazini katika sanaa ya ufundi lakini kutokana na hali ya hewa ya nchi hiyo ilibidi arudi nyumbani Tanzania kwa ajili ya kumalizia masomo katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Mwaka 1974  hadi 1976 alifanya kazi ndani ya Wizara ya elimu kama mratibu wa vyuo vya ufundi Tanzania lakini kutokana na mapenzi yake katika ufundishaji aliomba serikali imrudishe katika ufundishaji.
“Mwaka 1976 hadi 1980 nilifundisha katika chuo cha ualimu  cha Mara. Na mwaka 1980 hadi 1984 nilikuwa nafundisha vyuo viwili , Kasulu na Kabanga vyote vipo mkoani Kigoma.

SIRI YA UMRI WAKE
Njovu anasema siri kubwa ya kuwa na umri wa miaka 86 ni mapenzi ya Mungu kumuweka mpaka sasa lakini pia ni kutokana na kujitunza kwake hususan katika maswala ya vyakula ambavyo vinamfanya azidi kuishi akiwa na afya njema na nguvu.
Anasema yeye hupendelea zaidi vyakula vya asili hasa mboga mboga zaidi mchunga na matunda.
Kingine ambacho ni kubwa zaidi katika kuimarisha afya katika umri wake wake huo Njovu anasema hutembea umbali kiasi cha kilometa 7 hadi 10 kwenda na kurudi, wakati akisambaza bidhaa alizotengeneza (mihuri) kwa wateja wake.
Njovu ambaye ni mkazi wa Kibamba hutemebea hadi Kibaha, Bagamoyo na vijiji jirani.

LUGHA
Licha ya Kiswahili ambacho n dio Lugha mama lakini Njovu anamudu kuzungumza lugha ya Kikorea, Kichina, Kiingereza pamoja na baadhi ya lugha za asili za makabila ya ukanda wa kaskazini na Kenya.

MAISHA YA NDOA
Njovu alifanikiwa kuoa mke ambaye kwasasa ni marehemu mwaka1964 ambaye pia alikuwa mwalimu na walibahatika kupata watoto 8 wasichana wanne na wavulana wanne hata hivyo anaishi peke yake kwa sasa kutokana na watoto wake wote kuwa wanajitegemea.
Licha ya kuwa na umri huo lakini Njau anasema kuwa anajipikia mwenyewe chakula kwani kwake ni suala dogo na ameshazoea kwa maidai kuwa alichelewa kuoa. 
Hata hivyo Njovu anasema pia alikuwa mwalimu wa muziki kama somo la ziada, fani ambayo aliimudu vizuri katika kuimba na kupiga ala za muziki zikiwemo kinanda, tarumbeta, na saxophone.
Njovu anamaliza kwa kutoa rai kwa vijana kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia sana katika maadili ya kijamii pamoja na kujali afya zao kwa kupenda kufanya mazoezi na kusoma vitabu mbalimbali ili kujiongezea maarifa

COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Njovu: Mwalimu msataafu anayeishi kwa kuchonga mihuri
Njovu: Mwalimu msataafu anayeishi kwa kuchonga mihuri
https://1.bp.blogspot.com/-DCOgEVgF8HQ/V77TVYNqDsI/AAAAAAAAALs/HZtFCBA629syOPMnxMzd2EIhAJ2wa8GpQCLcB/s400/Moja.JPG
https://1.bp.blogspot.com/-DCOgEVgF8HQ/V77TVYNqDsI/AAAAAAAAALs/HZtFCBA629syOPMnxMzd2EIhAJ2wa8GpQCLcB/s72-c/Moja.JPG
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2016/08/njovu-mwalimu-msataafu-anayeishi-kwa_25.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2016/08/njovu-mwalimu-msataafu-anayeishi-kwa_25.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy