$type=slider$snippet=hide$cate=0

Tunamtaka Rais anayekerwa na mzigo wa deni la taifa, misamaha ya kodi

Waziri wa fedha anayemaliza muda wake, Saada Mkuya                                         TAKWIMU zinaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi ...


Waziri wa fedha anayemaliza muda wake, Saada Mkuya
                                        TAKWIMU zinaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu deni la taifa lilifikia Shilingi trilioni 53 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 19 kutoka wastani wa deni la taifa la Sh.trilioni 6.7 mwaka 2005.
Wakati taifa likiandamwa na madeni, takwimu pia zinaonyesha kuwa kasi ya kukopa na misamaha ya kodi imekuwa kubwa kuliko ile ya kulipa deni la taifa. Kwa mfano kuanzia mwezi Julai 2014 hadi April mwaka huu, misamaha ya kodi ilifikia Sh. trilioni 1.3 sawa na asilimia 1.4 ya pato la taifa.


Pamoja na hayo yote, tunaambiwa kuwa katika mwaka huu wa fedha jumla ya Sh. trilioni 16 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida huku shughuli za maendeleo zikitengewa Sh.trilioni sita tu.
Aidha Serikali imekuwa ikilalamika kuwa baadhi ya wafadhili hawatekelezi ahadi zao za kuichangia bajeti, na hivyo kuilazimu Serikali kukopa fedha kutoka benki ili kuendesha mipango ya maendeleo.
Kwa mfano, Ilielezwa na wabunge wakati wa uwasilishaji wa bajeti ya mwaka 2012/13 kuwa katika bajeti iliyotangulia kabla ya mwaka huo wa fedha, takribani asilimia 40 ya fedha zilizotarajiwa kutolewa na wafadhili hazikupatikana.
                                                                           
Hivyo maana yake ni kwamba, miradi iliyopangiwa fedha za maendeleo kutoka kwa wafadhili haikutekelezwa kwa asilimia mia moja.
Hata hivyo, Serikali hiyo hiyo, ambayo asilimia 75 ya bajeti zake huelekezwa kwenye matumizi, imekuwa kinara wa kuendekeza misamaha ya kodi kwa makampuni makubwa na kulimbikiza deni la taifa. Kwa upande mwingine, wafadhili wanaoridhia kuichangia bajeti ya serikali, wamekuwa na masharti mbalimbali.
Mara kadhaa serikali ya Tanzania imekuwa ikipewa masharti na Shirika la Fedha Duniani (IMF), la kuhakikisha kuwa inaweka umakini mkubwa katika kukusanya kodi na kutii misingi ya Utawala Bora.
Tunapoelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, wananchi wanao wajibu wa kuwahoji wanasiasa kujua fedha zinazo kopwa zinaztumikaje? misingi ya kukithiri misamaha ya kodi kwa makampuni ya uwekezaji na ulegevu wa mifumo ya ukusanyaji kodi.
Kwa kiwango cha misamaha ya kodi kinavyopaa na deni la taifa kuzidi, Tanzania inahitaji Serikali ya awamu ya tano kuwa makini na ukusanyaji kodi, mipango madhubuti ya kutolimbikiza deni la taifa.
Kuna ulazima kwa Watanzania kujua mchanganuo wa matumizi wa fedha zinazokopwa iwapo ni kwa shughuli za maendeleo ama matumizi ya posho, ziara, semina, mishahara na mambo mengine yanayohitaji serikali kuwa wazi (Open Government).
Mgombea urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Anna Mghwira
Misamaha ya kodi iliyotolewa kwa mashirika na makampuni binafsi, iliikosesha serikali mapato y a Sh. trilioni 1.03 kwa mwaka wa fedha 2011/12.
Katika Taarifa ya Utafiti ya mwaka 2010, iliyotolewa na taasisi iliyoitwa `The One Billion Dollar Question’, inaonyesha kuwa kabla ya bajeti ya mwaka 2011/12,Tanzania ilikuwa imepoteza takribani Sh. trilioni 1.7 kutokana na misamaha ya kodi,ukwepaji wa kodi, udanganyifu kwenye biasha ya kimataifa na utoroshwaji wa mitaji nje.
Udhaifu katika kukusanya mapato uliifanya serikali kukosa fedha za kutosha kutekeleza bajeti ya sh trilioni 13 iliyoidhinishwa na Bunge kwa mwaka wa fedha 2011/12.
Hadi kufikia 2011/12, Deni la taifa lilikuwa sh trilioni 22 kutoka sh trilioni 13 ya mwaka 2010/11, kutokana na serikali kukopa kwenye Benki za Biashara na Shirika la Fedha Duniani.
Suala la kutokukusanya kodi ipasavyo, linamuongezea mzigo mwananchi wa kawaida kupitia bidhaa za lazima anazotumia, kupanda bei kila leo na makato lukuki kwa wafanyakazi ukilinganisha na kiwango cha mishahara yao.
Mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa
Katika bajeti ya mwaka 2012/13 iliyoelekezewa Sh. trilioni 15.Trilini 10 zilitengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo zilitengewa Sh. trilioni tano tu. Bajeti ya mwaka 2012/13 pia ilionyesha kuwa, serikari ilitarajiwa kukusanya Sh. trilioni 8.7 kama makusanyo ya kodi ya ndani ambapo ilipanga kutumia Sh. trilioni 10.6 kwa matumizi ya kawaida. Kwa mchanuo huu, Serikali ilikuwa lazima itumie fedha ya mkopo kwa matumizi ya kawaida. Katika bajeti hiyo hiyo, Serikali iliainisha kuwa ilitakiwa kukopa Sh. trilioni 5.
Ripoti iliyotolewa mwezi Oktoba mwaka jana na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ilisema kuwa misamaha mikubwa ya kodi ilisababisha pengo la asilimia 10 ya bajeti ya mwaka wa fedha 2012/13. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, iliyowasilishwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC), misamaha ya kodi ilikuwa ni zaidi ya trilioni 1.5 sawa na asilimia 10 ya bajeti ya mwaka huo iliyoelekezewa Sh. trilioni 15.191.
Fedha zinazopotea kupitia misamaha ya kodi ni kubwa kuliko fedha zinazotolewa na wahisani.Kwa mfano, katika bajeti ya mwaka 2012/13, fedha zilizotolewa na wahisani zilikuwa sh trilioni 1.3.
Hii inamaanisha kwamba, fedha hizo Serikali isingeweza kuzikopa iwapo tu isingeendekeza misamaha ya kodi kwa sababu ingekuwa nayo mfukoni.
Kwa kukokotoa, Sh trilioni 1.5 iliyopotea ingeweza kusaidia upatikanaji wa huduma nyigine za jamii.Kwa mfano kama dawati moja la kiwango cha juu, linakadiliwa kuwa na thamani y ash 140,000/=,fedha hii ingeweza kutumika kununulia madawati zaidi ya milioni 10 na hivyo kumaliza kabisa tatizo hilo kwa shule nyingi nchini.
Ni aibu kubwa kwa nchi yenye rasilimali nyingi kuzungumzia uhaba wa madawati kwa kipindi cha zaidi ya miaka 50 tangu uhuru.
Aidha, fedha hizo zingeweza kutumika kugharimikia uchimbaji wa visima virefu vya maji, kuimarisha miundombinu ya barabara, kujenga zahanati zakutosha na pia kumaliza tatizo la mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini.
Kwa upande mwingine, kama Sh. trilioni 1.5 zimgekusanywa kupitia mfumo wa kodi, zingeweza kutumika kukamilisha ujenzi wa maabara zenye thamani ya wastani wa Sh. milioni mia moja kwa kila moja.
Serikali isingekuwa inaumiza kichwa tena kwa tatizo hili linazozikabili shule nyingi na wananchi wasingesumbuliwa kwa michango ya miradi hiyo, kwani fedha hizo zingetosha kukamilisha ujenzi wa maabara 15,000.
Mwaka 2012 takwimu zinaonyesha kuwa deni la taifa liliongezeka kwa asilimia 15.2 ndani ya mwaka mmoja wa fedha kutoka Sh. bilioni 18.2 mwaka 2011 na kuwa bilioni 21 mwaka 2012.
Kati ya fedha hizo deni la fedha za nje lilikuwa asilimia 75.95. Sababu iliyoelezwa na serikali kuwa lilitokana na mikopo mipya kwa ajili ya kugharimikia barabara, umeme na malimbikizo ya riba ya mikopo ya nyuma.
Serikali ilitenga sh trilioni 19.7 kwa ajili ya bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15. Sehemu kubwa ya bajeti hiyo ilitengwa kwa ajili ya kugharimikia uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014, maandaalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu na kukamilisha rasimu ya katiba mpya.
Bajeti hiyo ilikuwa na ongezeko la sh trilioni 1 toka bajeti ya mwaka 2013/14.
Akiwasilisha bajeti ya serikali bungeni ya mwaka 2015/16,Waziri wa fedha,Saada Mkuya Salum alisema,serikali imeweka mapendekezo kwenye muswada wa fedha wa mwaka 2015/16,wa namna ya kutambua wawekezaji mahususi wa kimkakati ambao watapewa misamaha ya kodi itakayo pendekezwa na waziri wa fedha ili kupata idhini ya bunge.
Sifa za mwekezaji huyo ni kuwa na mtaji usiopungua dola milioni 300 za Marekani na mtaji wa kifedha unapaswa upitie kwenye taasisi za fedha zilizopo nchini.
Pamoja na uwekezaji wake huo utoe ajira kwa watanzania wasiopungua 1,500. Katika bajeti hiyo, serika liimekadilia kutumia sh trilioni 22.495, ambazo ni Sh. trilioni 16.576 kwa ajili ya matumizi ya kawaida, wakati shughuri za maendeleo zimetengewa Sh. trilioni 5.919 ambazo ni idogo kuliko fedha zitakazokopwa kufidia nakisi katika bajeti.
Waziri wa fedha, Saada Mkuya, wakati akiwasilisha bajeti hiyo, alisema serikali inatarajia kukopa kutoka katika vyanzo vya ndani nan je kiasi cha Sh. trilioni 6.175 ili kuziba nakisi inayotokana na kiwango kikubwa cha matumizi ikilinganishwa na mapato.
Wakati serikali ikijipanga kupata kiasi hicho cha fedha, waziri Mkuya aliliambia Bunge kuwa hadi machi mwaka huu, deni la taifa lilikuwa limefikia dola za Marekani bilioni 19.5 sawa na Sh. trilioni 35. Fedha ambazo zinatosheleza kugharimikia bajeti nzima ya mwaka 2015/16 na kubaki, ikilinganishwa na Sh. trilioni 30.6 machi 2014 ya deni la taifa.
Licha ya waziri Mkuya kusema serikali imeendelea kupunguza utegemezi wa bajeti kutoka asilimia 24 mwaka 2004/05, asilimia 17 mwaka 2010/11 na kufikia asilimia 6.4 mwaka 2015/16.
Ukweli unabaki kuwa haauna faida yoyote ikiwa zimetengwa fedha nyingi za bajeti kwa ajili ya matumizi na zile za shughuli za maendeleo kusuburi fedha za wahisani.
IMETUMIKA:TAIFA LETU
==========

COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Tunamtaka Rais anayekerwa na mzigo wa deni la taifa, misamaha ya kodi
Tunamtaka Rais anayekerwa na mzigo wa deni la taifa, misamaha ya kodi
http://2.bp.blogspot.com/-bC6sthjKVhI/VfASZe0EJPI/AAAAAAAAAHU/XSO4n3PcPhk/s400/Mkuya.jpg
http://2.bp.blogspot.com/-bC6sthjKVhI/VfASZe0EJPI/AAAAAAAAAHU/XSO4n3PcPhk/s72-c/Mkuya.jpg
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/tunamtaka-rais-anayekerwa-na-mzigo-wa.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/tunamtaka-rais-anayekerwa-na-mzigo-wa.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy