$type=slider$snippet=hide$cate=0

Sheria makosa ya mitandao inapoanza kuwa muhimu uchaguzi mkuu

SHERIA ya makosa ya mitandao ilianza kutumika Septemba Mosi, mwaka huu baada ya kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tan...





SHERIA ya makosa ya mitandao ilianza kutumika Septemba Mosi, mwaka huu baada ya kupitishwa na Bunge la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na kusainiwa na Rais Jakaya Kikwete.

Baada ya hatua ya rais kuisaini sheria hiyo maana yake sasa usimamizi wa utekelezaji wa sheria hiyo utasimamiwa na vyombo vya dola yaani Jeshi la Polisi na Mahakama.
Sheria hiyo kabla ya kusainiwa na kuanza kutumika ililalamikiwa na makundi mbalimbali ya jamii na kuzua mjadala mkali miongoni mwa wananchi, ambao wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kwa shughuli zao mbalimbali za kila siku.
 Kubwa zaidi ni kuwa makundi hayo yalilalamikia hatua ya serikali ya kufanya maandalizi bila ushirikishaji wa jamii kupitia wadau ili watoa maoni yao kuhusiana na jinsi gani sheria hiyo iwe; kwa maana ni mambo gani yaingizwe kadri wangeona inawafaa.
 Kutokuwashirikisha wadau kulitafsiriwa kwamba serikali haikuwa na nia njema, bali nia ovu ambayo lengo lake ni kudhibiti uhuru wa jamii kupashana habari, jambo ambalo ni haki ya msingi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Tunapozungumzia haki ya kupeana taarifa maana yake ni kwamba jamii iwe huru kutumia vyombo vya mawasiliano zikiwamo redio, televisheni, magazeti, majarida na mitandao ya kijamii ilimradi sheria za nchi zifuatwe.
 Ili kuhakikisha kuwa vyombo hivyo vinatumiwi vibaya kukiuka sheria na kuingilia uhuru wa watu binafsi, ndiyo maana serikali ilitunga sheria kuanzia ya magazeti ya mwaka 1976 na ya utangazaji ya mwaka 1993.
 Hizi sheria hususan ya magazeti ambayo imekuwa ikitekelezwa sambamba na Sheria ya Usalama wa Taifa namba 20 ya mwaka 1970 kwa miaka mingi, imekuwa ikilalamikiwa sana kutokana na kumpa Waziri mamlaka makubwa ikiwamo kulifungia gazeti lolote kwa muda usiojulikana bila hata kusikiliza utetezi.
 Sheria hiyo iliorodheshwa na Tume ya Nyalali ya mwaka 1991 kuwa ni miongoni mwa sheria mbaya ambazo zilipaswa kufutwa, lakini hadi leo serikali imekaa kimya na inaendelea kutumiwa kufungia magazeti.
Kuna orodha ndefu ya magazeti ambayo waziri aliyafungia kwamuda usiojulikana na mengine kupewa amri ya kusimamisha uchapishaji kwa miezi kadhaa kwa maelezo ya kukiuka maadili, lakini bila kupewa haki ya kuwasilisha utetezi.
 Tume ya Jaji Nyalali ilisema sheria hiyo na nyingine zipatazo 40 zimepitwa na wakati, hivyo zifutwe kwa sababu hazifai kutumika katika nchi ya kidemokrasia inayofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Sheria ya Makosa ya Mitandao ina maeneo kadhaa ambayo lengo lake ni kudhibiti matumizi mabaya. Miongoni mwa maeneo yanayoguswa nasheria hiyo ni pamoja na kusambaza ujumbe wa uchochezi kupitia mitandao ya kijamii.
Serikali iliandaa sheria hiyo kwa kueleza kuwa ina lengo la kudhibiti matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ikiwamo ya Watsapp, Facebook, Youtube, Instagram na mingine.
Pamoja na maelezo hayo ya serikali kwamba lengo la kutungwa kwa sheria hiyo ni mazuri, lakini makundi kadhaa ya jamii hayakuridhishwa na maelezo hayo na kuendelea kuhoji kuhusiana na kuandaliwa kwa sheria hiyo pamoja na kusainiwa na rais kuwa sheria kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika  Oktoba 25 mwaka huu.
Kuna watu wanaamini kuwa lengo la sheria hiyo ni kudhibiti uhuru wa maoni ya wananchi na hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi huo wa rais, wabunge na madiwani. Katika mazingira hayo, hisia za watu hao hazipaswi kupuuzwa kutokana na uzoefu ulioko nchini; kwamba wakati wa uchaguzi maamuzi mengi ya ghafla na ya kushangaza hufanyika na kuzua maswali katika jamii.
 Watu hao wanaamini hivyo kutokana na moja ya vifungu vya sheria hiyo kupiga marufuku ujumbe wa uchochezi ama ushawishi wa kisiasa unaoweza kuleta athari kwa jamii kupitia mitandao.
Pia, sheria hiyo inabana kuhusu masuala ya kusambaza au kutunga ujumbe unaoleta uchochezi wa kidini unaoweza kusababisha kuvuruga amani na maelewano ndani ya jamii kupitia mitandao.
Sheria hiyo inaeleza wazi kwamba wavunjaji wa sheria husika wanaweza kukabiliwa na vifungo vya gerezani au faini ya fedha isiyopungua Shilingi milioni tano kulingana na kosa lililofanyika.
Kutokana na ukweli kuwa sheria yenyewe ilishapitishwa na wabunge, ni vizuri sasa Watanzania wakazingatia utekelezaji wake ili kujiepusha adhabu zilizoainishwa.
Mathalan,matumizi ya mitandao yamekuwa ya kiwango cha juu katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Mitandao hiyo imekuwa ikitumika kwa njia mbalimbali zikiwamo kampeni miongoni mwa wagombea, lakini pia kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiitumia kuwashambulia, kuwakashifu, kuwatukana, kuwatisha wenzao na mambo mengine ya ovyo.
Kadhalika, mitandao hiyo imekuwa ikitumika vibaya na kuwazushia mambo, kuwatukana na kuwadhalilisha watu mbalimbali wakiwamo viongozi wa kitaifa.
Pamoja na ukali wa sheria yenyewe, ni vizuri wananchi wakaisoma na kuielewa sheria hiyo ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kuwakuta huko mbele ya safari.
Sheria hiyo ni kali na inadhibiti baadhi ya maeneo na hasa yale ya utoaji wa maoni, lakini sisi kama taifa inabidi tukubali kuwa taifa letu katika kipindi hiki linahitaji miongozo ya kudumisha amani na utulivu.
 Kimsingi, lengo la kuanzishwa kwa mitandao ya kijamii ni zuri kwa lengo la kupashana habari kwa urahisi, lakini kwa bahati mbaya sana, baadhi ya watu wamebadili matumizi yake.
 Siku hizi mitandao ya jamii imegeuzwa kuwa sehemu ya kuzushia watu mabaya. Si ajabu kusoma kwenye mitandao kuwafulani kafa wakati ni uongo. Nakumbuka kuna siku mtandao mmoja ulidai kuwa mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, amefariki dunia wakati haikuwa kweli.
Mara kadhaa katika mitandao zimekuwa zinaandikwa habari za uzushi kuhusu kutokea kwa ajali za barabarani wakati siyo kweli.
 Hivi karibuni, mtandao mmoja uliandika kuwa Makamu waRais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alikuwa na mkutano na vyombo vya habari katika moja ya hoteli za kitalii, jijini Dar es Salaam kuelezea hatma yake ya kisiasa wakati haikuwa kweli.
 Katika mazingira kama haya, nchi haiwezi kwenda wala kutawalika, ni lazima mitandao itumike pamoja na mambo mengine, kuheshimu uhuru wa watu, haki, faragha na kuhakikisha kuna amani na utulivu wa nchi.
 Kwa kuwa tayari muswada uliokuwa unalalamikiwa na wadau umeshakuwa sheria, ni muhimu sana kwa wananchi kuisoma vizuri sheria hiyo na kuielewa kwa kuwa atakayefanya makosa atashughulikiwa bila kusamehewa kwa kuwa kutojua sheria siyo utetezi (ignorance of law has no defence).
Sheria ikishasainiwa kinachobakia ni utekelezaji wake, kila mmoja ahakikishe anajiepusha na kitendo chochote ambacho kitakiuka sheria hiyo kwa kuwa matokeo yake itakuwa ni kufungwa jela au kutozwa faini.
 Kwa kuwa serikali ilishasema kuwa kama yataonekana mapungufu wakati wa utekelezaji wake itakuwa tayari kuipitia, ni vizuri itekeleze ahadi hiyo kwa kuwa upitishaji wake uliacha maswali mengi kuliko majibu kutoka kwa wananchi.
 Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, aliyetoa ahadi hiyo hanabudi kuhakikisha utaratibu wa kupata maoni ya wadau unaanzishwa ili kuangalia uwezekano wa kuiboresha sheria hiyo itekelezwe bila kuwapo malalamiko na manung’uniko kutoka kwa jamii.
IMETUMIKA TAIFA LETU

COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Sheria makosa ya mitandao inapoanza kuwa muhimu uchaguzi mkuu
Sheria makosa ya mitandao inapoanza kuwa muhimu uchaguzi mkuu
http://4.bp.blogspot.com/-6hq0vPHWnG0/Vflrh-UtTcI/AAAAAAAAAIM/o0zt-D3YJpM/s400/Sheria.jpg
http://4.bp.blogspot.com/-6hq0vPHWnG0/Vflrh-UtTcI/AAAAAAAAAIM/o0zt-D3YJpM/s72-c/Sheria.jpg
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/sheria-makosa-ya-mitandao-inapoanza.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/sheria-makosa-ya-mitandao-inapoanza.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy