$type=slider$snippet=hide$cate=0

Marais wetu wanapo pokezana `kijiti’ cha mgawo wa umme

Mkurugenzi wa Tanesco, Felchesmi Mramba  NISHATI ya umeme limekuwa ni tatizo ambalo limewaathiri Watanzania kwa miaka mingi bila k...



Mkurugenzi wa Tanesco, Felchesmi Mramba

 NISHATI ya umeme limekuwa ni tatizo ambalo limewaathiri Watanzania kwa miaka mingi bila kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Shida ya umeme ilianza kuitikisa nchi tangu uongozi wa awamu ya pili ya Ali Hassan Mwinyi na kurithiwa na awamu ya tatu ya Benjamin Mkapa ambaye naye alimrithisha Rai wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete.
 Rais Kikwete naye analiacha tatizo hilo kwa rais wa awamu ya tano ambaye atajulikana mwishoni mwa Oktoba mwaka huu baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25.

 Kutokana na tatizo hilo, serikali zote zimejaribu kuchukua hatua ikiwamo kuingia katika mikataba na kampuni mbalimbali za kufua umeme wa dharura.
 Kwa mfano, serikali ya awamu ya pili iliingia katika mkataba na Kampuni ya International Power Tanzania Limited (IPTL) mapema miaka ya tisini kwa lengo la kunusuru hali hiyo.
 Hata hivyo, pamoja na mkataba huo kuonekana kuwa wa kinyonyaji na kuibua malalamiko kuwa serikali haikuwa makini wakati wa kusaini mkataba huo, bado matatizo ya nishati hiyo yaliendelea.
 Moja ya kuongezeka wka mahitaji hayo ni kutokana na mvua kutokuwa za uhakika na kusababisha mabwawa yaliyojengwa kwa ajili ya kuzalisha umeme kukauka mara kwa mara.
 Adha ya kukauka kwa mabwawa ya Mtera, Kidatu, Nyumba ya Mungu na mengine imekuwa ikishuhudiwa mara kwa mara pale mvua zinapokosekana au kunyesha kwa kiwango kidogo.
 Kwa mfano, mwaka 2006 nchi ilikumbwa na janga kubwa la ukame lililosababisha kukauka kwa mabawawa na kutishia nchi kuingia gizani. Serikali iliamua kuingilia kati haraka kwa kuingia katika mkataba mwingine na kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond ya Marekani.
 Ingawa kampuni hiyo ilibainika kuwa haikuwa na uwezo wa kuzalisha umeme na kwamba ilipewa zabuni kwa upendeleo, lakini ilipewa zabuni ya kuzalishamegawati 100 kwa gharama ya takribani Shilingi bilioni 180. 
Sina lengo la kujadili masuala ya IPTL wala Richmond ambayo yamegeuzwa siasa, lakini ninachotaka kueleza hapa ni jinsi gani Watanzania wanaendelea kuumizwa na tatizo la umeme bila sababu za msingi.
 Ingawa baada ya serikali kujikita katika uchumi wa gesi; kwa maana ya kuanza kuitumia kama chanzo cha nishati, Watanzania wameanza kujenga matumaini ya kuondokana na adha hiyo, lakini bado serikali inawasababishia adha bila sababu za msingi.
 Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Jumapili iliyopita, lilitangazia umma kwamba nchi nzima itakuwa gizani kwa takriban wiki nzima kuanzia Jumatatu.
 Shirika hilo lilieleza kuwa hali hiyo inatokana na kuzimwa kwa mitambo ya gesi inayozalisha umeme kutoka Songosongo mkoani Lindi.
 Kwa mujibu wa Tanesco, lilichukua hatua hiyo kutokana na kazi ya kuunganisha bomba la gesi kutoka Mtwara na mtambo wa umeme wa Kinyerezi II.
 Hatua hiyo ilianza kuwaathiri wananchi kuanzia Jumatatu baada ya baadhi ya mitambo ya kuzalisha nishati hiyo kuzimwa kwa ajili ya kutekeleza  kazi hiyo.
 Uamuzi wa Tanesco pamoja na kwamba ni mchungu kwa watumiaji wote wa umeme, lakini dhamira yake  njema na lengo lake ni kuboresha utoaji huduma ya umeme nchini ambayo kwa miaka nenda rudi, imekuwa haikidhi matarajio ya wateja wake na Watanzania kwa ujumla.
Hata hivyo, Tanesco hawakutumia busara sana katika kutekeleza kazi hiyo kwani hawakushirikisha wateja wao na umma kwa ujumla.
 Dunia ya leo inaendeshwa  kwa uwazi na ushirikishaji, hivyo Tanesco ilipaswa kuwashirikisha wateja wake na umma kwa ujumla kwa kuwapa taarifa mapema kwa kuwa kazi ya kuunganisha bomba la gesi kutoka mkoani Mtwara na mitambo yake, ilikuwa imepangwa kwa muda mrefu. 
Kazi hiyo haikuwa ya dharura, lakini wateja na umma ulijulishwa kwa dharura yaani siku mpja kabla ya kazi hiyo kuanza kutekelezwa.
Kwa nini taarifa isingetolewa mwezi mmoja kabla ili watumiaji wa umeme wajiandae kuchukua hatua za kukabiliana na athari ya kukosa umeme kwa wiki nzima?
 Watumiaji wa umeme wanatofautiana katika matumizi ya nishati hiyo kwa kuwa kuna wamiliki wa viwanda vikubwa, viwanda vidogo, taasisi, wafanyabiashara na watumiaji wa kawaida.
 Wote hao kila mmoja alitakiwa kupewa taarifa mapema akajiandaa kwa kupanga bajeti yake. Wapo ambao wangehitaji kununua jenereta, mafuta ya kuendesha jenereta, kununua taa, mishumaa na vifaa vingine ili kuhakikisha kwamba shughuli zao hazikwazwi kwa kukosa umeme kwa wiki nzima.
Katika muktadha huo, shirika hilo lingetakiwa kutoa taarifa ili wahusika wajipange kwa ajili ya kukabiliana na makali hayo.
Wamiliki wa viwanda wana mahitaji makubwa ya umeme na nishati hiyo ndiyo inayowezesha viwanda vyao kuzalisha, hivyo walihitaji taarifa ya muda mrefu ili wafanyie matengenezo  jenereta zao.
 Mbali na viwanda ambavyo kwa asilimia kubwa hutegemea umeme wa shirika hilo, lakini pia wajasiriamali mbalimbali hutegemea nishati ya umeme kuendeshea shughuli zao za kiuchumi kama vile saluni za kike na kiume, inateneti, gereji za magari, wauzaji wa vinywaji baridi na vikali, wauza samaki, juisi, na nyama, mama ntilie, wachomeleaji vyuma; kutaja baadhi.
Aidha, hatua hii ya Tanesco kwa kiasi kikubwa pia itaathiri uzalishaji wa viwandani kwani vitalazimika kuingia gharama za kutumia majenereta yanayotumia mafuta.
 Matumizi ya jenereta, ni wazi kwamba yatachangia kwa kiasi kikubwa kupandisha bei ya bidhaa zinazozalishwa viwandani na hivyo kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi.
 Viwanda vingi vinaendeshwa kwa bajeti na hatua hii ya Tanesco kuzima ghafla mitambo yake, italeta athari kubwa.
Mbali na shughuli hizo za kiuchumi, lakini pia kuna masuala ya kijamii kama shughuli za hospitali kwani kwa hatua hii ya Tanesco, ni dhahiri wagonjwa wengi wanaohitaji huduma za matibabu wataathirika.
Kwa kuwa Watanzania bado wanakumbuka adha ya umeme ya muda mrefu, ni vizuri wangepunguziwa mzigo wa mgawo wa umeme kwa kupatiwa taarifa ya muda mrefu.
Wengi wetu tunaunga mkono mipango ya Tanesco ya kuboresha huduma za umeme nchini ikiwamo kuwakumbuka wananchi wa vijijini kupitia Mradi wa Umeme Vijijini (Rea), lakini
 Kitu cha muhimu na cha msingi ni kwamba Watanzania wanapaswa kujengewa mazingira ya kusahau kero za nishati ya umeme hususani mgawo uliowatesa kwa nyingi.
Kwa kuanzia kuna haja kwa shirika kuanzia utaratibu wa kutoa taarifa mapema kwa umma kuhusiana na kuwapo kwa mgawo wa umeme pale kutakapokuwapo na matengenezo au kuunganisha bomba la gezi katika Grid ya Taifa, ambayo ni tegemeo la maeneo mengi ya nchi kupata umeme.
Watanzania kwa muda mrefu walibeba mzigo wa umeme kiasi kwamba nishati hiyo imegeuka kuwa huduma ya upendeleo kwa walio wengi badala ya kuwa ya lazima kwao.
IMETUMIKA: TAIFA LETU
=======


COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Marais wetu wanapo pokezana `kijiti’ cha mgawo wa umme
Marais wetu wanapo pokezana `kijiti’ cha mgawo wa umme
http://4.bp.blogspot.com/-UjXgWOi2j1Q/VfAU7XaPv4I/AAAAAAAAAHg/rNuCbEzKAAY/s400/Mkurugenzi%2Bwa%2BTanesco%2Bfelchesmi%2BMtramba.jpg
http://4.bp.blogspot.com/-UjXgWOi2j1Q/VfAU7XaPv4I/AAAAAAAAAHg/rNuCbEzKAAY/s72-c/Mkurugenzi%2Bwa%2BTanesco%2Bfelchesmi%2BMtramba.jpg
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/marais-wetu-wanapo-pokezana-kijiti-cha_9.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/marais-wetu-wanapo-pokezana-kijiti-cha_9.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy