$type=slider$snippet=hide$cate=0

Jeshi la Polisi likomeshe vikundi vyote vya kulinda kura

IGP Ernest Mangu MAPEMA wiki hii, Jeshi la Polisi kupitia Mkuu wa Jeshi hilo (IGP), Ernest Mangu lilisisitiza onyo dhidi ya vya...




IGP Ernest Mangu
MAPEMA wiki hii, Jeshi la Polisi kupitia Mkuu wa Jeshi hilo (IGP), Ernest Mangu lilisisitiza onyo dhidi ya vyama vya siasa, wagombea na wafuasi wa vyama hivyo kujiepusha na vitendo vitakavyokiuka taratibu za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
 Katika Mkutano wake na viongozi mbalimbali wa dini na kisiasa, IGP alisema vyombo vya usalama vimejipanga vyema kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu unafanyika kwa amani na utulivu licha ya vuguvugu la ushindani mkali wa kisiasa uliopo.

Alivitaja vyama vya siasa vya Chama cha Mapinduzi (CCM) na vyama vya upinzani kama vya muungano wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vya NCCR-Mageuzi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), NLD na Chama cha Wananchi (CUF) kuwa na ushindani mkubwa wa kisiasa lakini pamoja na uwepo wake, jeshi la polisi halitarajii kuvunjika kwa amani na utulivu kwa namna yoyote ile.
Ni wazi kwamba kauli ya kiongozi  huyo mkuu wa jeshi ni tahadhari anayoitoa kwa mamlaka za vyama kuwa makini, utiifu, na ni wazi kwamba kauli yake hiyo pia ni ombi kwa viongozi wa dini kutumia nyumba za ibada kuwahamasisha waumini wao ili kujiepusha na vurugu wakati wa uchaguzi mkuu.
Hii maana yake ni kwamba watakaovunja sheria, watashurutishwa kutii sheria jambo ambalo kwa uzoefu tunaoupota katika nchi za jirani ni wazi kwamba ushurutishaji wa sheria umeleta madhara makubwa ikiwamo vurugu, vita, vifo na wananchi wengine kulazimika kuyakimbia makazi yao.
Tumeshuhudia kwa kuona, kusikiliza na kusoma kwenye vyombo mbalimbali vya habari 0kuwa waathirika wakubwa wa matukio ya fujo na vita ni wanawake, watoto, walemavu na kundi  la watu wengine wasiojiweza kama vile wazee.
Tunapohimiza kufanyiwa kazi kwa onyo la jeshi la polisi, ni pale IGP Mangu anapotoa karipio hilo tunasikia kwamba wapo viongozi wa  vyama wanaohamasisha  mpango wa kuanzisha vikundi vya ulinzi vya vyama vya siasa kwa madai ya  kulinda kura wakati wa uchaguzi wakati kimsingi jukumu hilo lipo chini ya jeshi la polisi lenyewe.
Maana ya IGP kukemea vyama vya siasa vyenye malengo hiyo ni kusisitiza wajibu wake kwa jamii kwamba ni kulinda usalama wa mali na raia wakati na baada ya uchaguzi,  hivyo hakuna sababu yoyote ya vyama hivyo kuwa na vikundi  kama vile Green Guard  cha CCM, Blue Guard cha Chama cha Wananchi (CUF) na Red Brigade cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), na hivyo vyama vinapaswa kusitisha harakati zao kwani ni kinyume cha sheria. 
Sisi tunaungana na Jeshi la Polisi kukema vitendo vya vyote vinavyokiuka taratibu za uchaguzi kutokana na ukweli kwamba vyama hivyo hivyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na vyombo vya usalama vilikubaliana kwa kutiliana saini mambo ya kuzingatiwa wakati wa kampeni hadi uchaguzi mkuu ikiwamo chama, mgombea au wafuasi wake kutokiuka sheria na taratibu za uchaguzi na kusababisha kutoweka kwa amani na utulivu nchini.
Mojawapo ya mambo yaliyoanishwa na kukubaliwa ni pamoja na kutotumika kwa lugha za uchochezi kwama vile zinazoshinikiza ushindi, kuchana mabango ya mgombea wa chama kingine na matusi.
Lakini hata baada ya makubaliano hayo tumeshuhudia matumizi ya lugha za kuudhi, kuchanwa kwa mabango ya wagombea, vitisho na wagombea kujielekeza katika kusemana wawapo kwenye majukwa ya kampeni kutoa hoja zitakazowavuta wananchi ili kuwa rahisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Hii yote ni  kufanyika kwa kampeni zisizokuwa za ustaarabu ambazo kwa namna nyingine huweza kusababisha kukosekana kwa amani na utulivu siyo tu wakati huu wa kampeni isipokuwa inaweza kutumika kama nongwa wakati wa uchaguzi na kuchafua hali utulivu.
Sisi tunaamini kwamba kila mmoja ana wajibu wa kulinda amani na utulivu wa nchi yetu katika kipindi chote cha kampeni na siku ya uchaguzi mkuu hadi kutangazwa kwa washindi wa nafasi mbalimbali za uongozi walizoomba wagombea husika.
Hiyo ni pamoja na kutojihusisha na vikundi vyovyote ambavyo jeshi la polisi limeonya uwepo wake, vinginevyo jeshi la polisi litalazimika kutumia nguvu kutoa shuruti jambo ambalo ni hatari kwa usalama na mali zetu.
Pia tunakema tabia ya Watanzania wanaopenda hulka ya kushurutishwa kutii sheria bila kuzingatia msingi wa utii wa sheria bila shuruti.

CHANZO: TAIFA LETU
======

COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: Jeshi la Polisi likomeshe vikundi vyote vya kulinda kura
Jeshi la Polisi likomeshe vikundi vyote vya kulinda kura
http://4.bp.blogspot.com/-fg4pYrlg0Ew/Vfgrp1VQ9lI/AAAAAAAAAH8/4w83bKrU8_8/s400/MANGU.gif
http://4.bp.blogspot.com/-fg4pYrlg0Ew/Vfgrp1VQ9lI/AAAAAAAAAH8/4w83bKrU8_8/s72-c/MANGU.gif
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/jeshi-la-polisi-likomeshe-vikundi-vyote.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/09/jeshi-la-polisi-likomeshe-vikundi-vyote.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy