$type=slider$snippet=hide$cate=0

CCM irejee zama za Mwalimu Nyerere, vinginevyo....

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana Na Komba Kakoa RAFU zinazoendelea kulalamikiwa na makada mbalimbali wa Ch...


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana


Na Komba Kakoa
RAFU zinazoendelea kulalamikiwa na makada mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni matokeo ya Mamlaka husika kuacha utaratibu wa enzi ya chama hicho wakati wa Muasisi wake na wa Taifa, Mwalimu Julias Nyerere na kuanzisha mfumo ambao ni wazi kwamba utazika chama hicho.
Rafu hizo zinalenga kunufaisha baadhi ya makada ambao kwa maslahi binafsi watangaza nia wasiokuwa wadilifu hutumia mbinu mbalimbali za kuwahujumu wapiga kura ili waweze kuwachaguwa.

CCM iliyokuwa katika uongozi wa Hayati Baba wa Taifa hili ni tofauti na CCM ya leo kwasababu mbalimbali ambao kimsingi ni wazi kwamba kipo kwa ajili ya kunufaisha baadhi ya makada.
Kwamba katika kipindi cha nyuma viongozi wa chama hicho walikuwa waadilifu na wenye kuwajibika ipasavyo katika nafasi zao tofauti na ilivyo kwa baadhi ya makada kujipenda wenyewe na hata kufikia hatua za kukashifiana wenyewe pamoja na chama hicho jambo ambalo halileti picha nzuri.
Mintarafu yangu kwa leo ni kuhusiana na gharama mbalimbali za uchaguzi ambazo watia nia hutakiwa kuchangia katika hatua mbalimbali ikiwemo kuchukua fomu pamoja na gharama za kuwezesha kampeni na uwakilishi.
Hapo awali chama kilibeba jukumu la kusimamia mchakato mzima wa uchaguzi kuanzia ngazi ya uchukuaji wa fomu, kampeni, ulipaji wa mawakala pamoja na kuwezesha usimamizi wa mambo yote katika utekelezaji wa shughuli hiyo.
Lakini leo mambo ni tofauti kwa uchukuaji wa fomu kwa nafasi ya urais wanatozwa kiasi cha shilingi milioni moja, Ubunge sh. Laki moja na ngazi ya Udiwani ikitegemeana na makubaliano ya makada wa kata husika.
Mbali na gharama hizo pia kuna michango ya kuwezesha kampeni ambapo mtia nia huyo huyo anapaswa kulipa  mawakala wake wanaosimamia mchakato wa kuhesabu kura hali ambayo inamnyonya na kumnyima haki Mtanzania mwenye sifa na nia ya kuwania nafasi ya uongozi kwasababu ya gharama hizo ambazo awali hazikuwepo.
Kwa upande mwingine uwepo wa michango hiyo ni furaha kwa makada wenye uwezo hasa zaidi waliokuwa kwenye madaraka kwasababu wana marupurupu mengi yanayowafanya wamudu gharama hizo na kuwapa fursa ya kuwapiku wasiokuwa nacho.
Katika mchakato wa kura za maoni tuemeshuhudia mpasuko ndani (CCM) kutokana na uwepo wa makundi yaliyosababishwa na makada wenye uwezo kifedha na nguvu katika chama hicho jambo ambalo kimsingi halina tija kwa maendeleo na uwajibikaji katika kutekeleza ilani.
Yote hayo ni matokeo ya CCM kupitisha utaratibu wa mtangazania kugharimikia mchakato, swali linalosumbua vichwa vya Watanzania hasa wana CCM ni kwamba kwanini chama hicho kimeondoa ule utaratibu wa kubeba dhamana ya watia nia wote?
Kwamba katika wakati ule CCM ilibeba dhamana ya kufadhili watangazania wote kwa gharama zote za uchaguzi jambo ambalo liliimarisha chama na sote tulishuhudia umoja na uwajibikaji wa makada walipata fursa ya kuchaguliwa na kushika majimbo pamoja na kata mbalimbali hapa nchini.
Kutokana na utaratibu wa kila mtangazania kuchangia gharama za uchaguzi unaendelea kuleta madhara kwa wasionacho kufunikwa na kufanyiwa rafu za hapa na pale katika mchakato mzima wa kura za maoni.
Kwa makada waliotangaza nia walitembezwa pamoja kwa usafiri wa aina moja ili waweze kuonekana kwa wananchi na kupata fursa ya kujinadi na kuomba kura tofauti na ilivyo katika kipindi hiki ambacho kila mtia nia alisafiri kivyake na kwa utaratibu wake.
Katika kura za maoni tumeshuhudia makada wenye nacho wakikodisha mabasi na kuyabandika picha zao ‘stika’ na kuzunguka nayo sehemu mbalimbali kwa dhumuni la kujinadi.
Mbali na waliofanya hivyo wengine waliamua kukodisha vijana waendesha pikipiki `Bodaboda’ na kuwajazia mafuta na kuwapa kazi ya kuzunguka kwenye matawi ya CCM kwa lengo la kushawishi wapiga kura wawachague makada hao.
Mbali na hayo katika kufanya kampeni pia ni wazi kwamba katika kipindi cha nyuma hakukuwa na utaratibu wa kutangaza nia kwa makada jambo ambalo limeibuka na kusababisha baadhi ya makada kutumia mwanya huo kuanza kufanya kampeni kabla ya wakati.
Kwa hali hiyo ni vyema CCM ikarudia enzi yake na kuachana na mfumo ambao ni utazidi kudidimiza demokrasia ya nchi yetu pamoja na kuathiri zaidi watangaza nia wenye uchungu na changamoto za wananchi na kuwainua mabepari wenye uchu wa madaraka wanaodiriki kutumia rafu ilimradi tu wapate madaraka.
 
==============


COMMENTS

Name

HABARI,17,MAKALA,2,UCHAMBUZI,2,
ltr
item
TTAJA KIJIJI BLOG: CCM irejee zama za Mwalimu Nyerere, vinginevyo....
CCM irejee zama za Mwalimu Nyerere, vinginevyo....
http://4.bp.blogspot.com/-jR_oQ7BfpU8/VdsMZ7hbklI/AAAAAAAAADw/LSql8kaz82A/s400/Kinana.jpg
http://4.bp.blogspot.com/-jR_oQ7BfpU8/VdsMZ7hbklI/AAAAAAAAADw/LSql8kaz82A/s72-c/Kinana.jpg
TTAJA KIJIJI BLOG
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/08/ccm-irejee-zama-za-mwalimu-nyerere.html
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/
http://ttajakijiji.blogspot.com/2015/08/ccm-irejee-zama-za-mwalimu-nyerere.html
true
5988661810178760650
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy